Thursday, August 13, 2015

Polisi Wazuia Msafara wa LOWASSA Kushiriki Mazishi ya Mzee Kisumo


Polisi mjini Mwanga, mkoani Kilimanjaro umezuia msafara wa mgombea urais kupitia Chadema, Edward Lowassa uliokuwa unaelekea Usangi kuhudhuria mazishi ya kada wa CCM, Peter Kisumo.

TCRA Watoa ADHABU Kwa Kituo cha Televisheni cha ITV


Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) imetoa  adhabu ya onyo  kali  na  kukitaka  kituo cha  ITV kuomba radhi mara mbili mfululizo kwenye taariifa zake za habari baada ya kukiuka sheria ya utangazaji nchini ya Mwaka 2005.

Maandamano ya Kumpokea Edward Lowassa LEO Jijini Mbeya Yamepigwa MARUFUKU.


Jeshi la Polisi Mbeya limekataza maandamano ya Chadema ambao yalikua yafanyike leo Aug 14 wakati wa kwenda kumpokea Mwanachama mpya na Mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema Edward Lowasa.

Friday, August 7, 2015

Mke wa Dk Slaa afunguka......Akana Kumfungia Mumewe Chumbani


Siku moja baada ya Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa kuzungumza na kusema yupo salama, mke wake, Josephine Mushumbusi amekanusha tuhuma zilizozagaa kuwa ndiye aliyemshauri kiongozi huyo wa Chadema kujiuzulu na kumzuia kushiriki vikao muhimu vya chama.


Tetesi hizo zilivuma kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari baada ya Dk Slaa kutoonekana katika vikao muhimu vya Chadema na Ukawa, kuwa Mushumbusi hakupendezwa na kitendo cha Lowassa kupitishwa kuwania urais chini ya mwavuli wa Ukawa na badala yake alitaka Dk Slaa ndiye awe mpeperusha bendera.

Kwa mujibu wa taarifa hizo ambazo Mushumbusi amezikanusha, aliamua kumfungia ndani Dk Slaa kama moja ya mbinu za kumzuia asishiriki shughuli za kichama, tuhuma ambazo amezikanusha.

“Bosi wako akija kukuomba ushauri utamsaidia, lakini akija akakuambia ameshafanya maamuzi unaweza kupingana naye?” alihoji Mushumbusi akianza kutoa maelezo yake na kuendelea:

“Wakati wa vikao nilikuwa namwona (Dk Slaa) anachelewa kurudi kila siku, siku moja akaja akaniambia uamuzi aliouchukua na mimi sikuwa na la kusema, nikachukua shuka nikajifunika.”

Katika mahojiano yake ya kwanza  baada ya kuzagaa kwa tetesi hizo, Mushumbusi pia alikana kumfungia Dk Slaa ndani ya nyumba, akisema wakati maneno hayo yalipokuwa yanazagaa, alikuwa nje ya nchi na wala hakujua kinachoendelea.

“Mwenyewe najiuliza nini kinaendelea, siwezi kufanya kitu kama hicho. Nyumba yangu ina milango miwili, nawezaje kumfungia mtu, tena mwanamume, hata watoto siwezi kuwafungia. Kuna mambo mengine mwanamke huwezi kuyafanya kwa mwanamume. Mwanamume ni mwanamume tu,” alisema.

Alisema viongozi wa Chadema, ndugu, jamaa na marafiki walikuwa wanafika nyumbani kwake na walikutana na Dk Slaa na kuzungumza naye... “Kama ningekuwa nimemfungia wangezungumza naye vipi?”


Mushumbusi alisema mwanamke anaweza kufanya chochote lakini kuna baadhi ya mambo ambayo mwanamume akiamua ni vigumu kumzuia.

Akifafanua tuhuma za kumshinikiza Dk Slaa kujiuzulu Chadema, Mushumbusi alisema kiongozi huyo wa Chadema ana uamuzi wake na yeye ni msaidizi tu ambaye hana uamuzi wa mwisho kwenye familia.

Hata hivyo, alisema endapo angeamua kumshawishi, uwezo wa kufanya hivyo anao lakini yeye ni mwanamke mwadilifu anayependa mafanikio ya mumewe.

“Kwani unanionaje? Mimi ni ‘strong’ (nina nguvu), ningetaka ningefanya hivyo, nisingeshindwa,” alisema.

Pamoja na hayo, Mushumbusi alilalamika kuwa tuhuma hizo dhidi yake zimesababisha asisikilizwe kama ilivyokuwa awali.

Bila kufafanua kwa undani, alisema kuna kundi linalounda propaganda hizo ili abadili mtazamo kuhusu mumewe lakini jambo hilo haliwezi kutokea.

“Nilisema nitampenda kama alivyo, sitajali chochote wala akiwa katika hali gani au chama gani. Kazi yangu ni kumtia moyo ili kile atakachofanya kifanikiwe,” alisema.

Mbali na kukanusha vikali tuhuma hizo, Mushumbusi alisema alikwishajitoa kwenye masuala ya siasa kwa miaka miwili sasa na badala yake ameamua kufanya biashara ya kuuza mkaa.

“Nimenyamaza kimya, nimekaa kando ninaendelea na biashara yangu ya kuuza mkaa, nipo mbali na siasa na sitaki kujua kinachoendelea, kwanza hata mchakato wenyewe siujui,” alisema.

Aliwashauri wanawake kuacha kushabikia masuala yanayotokea ndani ya ndoa yake na kuwataka wavae viatu anavyovivaa na wajue kuwa anapitia wakati mgumu.

Profesa Lipumba Aondoka Nchini Akiwa Chini ya Ulinzi


Saa chache baada ya Profesa Ibrahim Lipumba kutangaza kujiuzulu wadhifa wa Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), ametoweka nchini.

Wasomi Wampuuza Profesa Lipumba.......Wasema Amekurupuka


Wasomi mbalimbali nchini, wamepokea kwa mtazamo tofauti uamuzi wa Profesa Ibrahim Lipumba kujiuzulu wadhifa wake wa Mwenyekiti wa CUF Taifa wengine wakisema suala hilo si jipya bali ni aina ya changamoto zilizopo kwenye vyama vya siasa nchini.

 
Wakizungumza na mtandao huu kwa nyakati tofauti, wasomi hao pia walimshangaa Prof. Lipumba kwa uamuzi huo kwani alishiriki tangu mwanzo katika kumpokea mgombea urais aliyepitishwa na Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), Bw. Edward Lowassa, tangu alipohama CCM na kujiunga na CHADEMA.
 
Dkt. Lazaro Swai wa OUT
Akizungumzia uamuzi huo, Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa na Jamii katika Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT), Dkt. Lazaro Swai, alisema anamshangaa Prof. Lipumba kwa uamuzi aliouchukua.
 
"Hizo ni aina ya changamoto zilizopo kwenye vyama vya siasa tangu vilipoanzishwa,  hilo ni shinikizo kutoka upande mmoja lakini si kutoka UKAWA wala CUF," alisema Dkt. Swai.
 
Aliongeza kuwa, hivi sasa katika vyama vya siasa kila mtu ana mvuto wa aina yake lakini kujiuzulu kwa Prof. Lipumba kutakuwa na mtikisiko kwa UKAWA na CCM kutokana na kuhama kwa Bw. Lowassa.
 
"Ujio wa Lowassa hauwezi kuipasua UKAWA, kujiuzulu kwa Lipumba kuna kitu ndani yake na kuleta mashaka kwa Watanzania, kwanini iwe sasa ndipo ajiondoe katika nafasi hiyo wakati alishiriki tangu mwanzo kumpokea Lowassa," alihoji.
 
Askofu Bagonza
Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Karagwe, mkoani Kagera, Benson Bagonza, alisema kujiuzulu kwa Lipumba kunaashiria kuna jambo nyuma ya pazia, kwani wananchi hawataelewa.
 
"Tangu mwanzo alikuwa msingi imara kwenye UKAWA, ghafla anajiuzulu hiyo inashangaza watu wengi na sitaki kuamini kama amefikia uamuzi huo," alisema na kuongeza;
 
"Kutakuwa kuna jambo jingine limetokea nje ya UKAWA lakini swali la kujiuliza, kwanini alichelewa kuchukua uamuzi huo...huyo si Lipumba tunayemjua," alisema.
 
Dkt. Benson Bana
Naye Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Idara ya Sayansi ya Siasa ya Jamii, Dkt. Benson Bana, alisema kujiuzulu kwa Prof. Lipumba kulitarajiwa kutokana na mvutano uliokuwepo tangu awali.
 

"Ameona ni wakati mwafaka kuachia ngazi pia ni haki yake ya msingi kwani ndani ya muungano wa UKAWA, hauwezi kumpokea mtu wakati  huo huo akawa maarufu kushinda chama.
 
"Hilo ni pengo la kudumu ambalo haliwezi kuzibika kwa siku moja, uamuzi wa Lipumba na Slaa utakuwa wa halali kwani waliwekeza sana kwenye vyama vyao," alisema na kuongeza kuwa, kiongozi yeyote anapimwa kwa uadilifu na walikuwa tayari kujitoa kafara katika nyadhifa zao.
 
Julius Mtatiro
Kwa upande wake, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara), Bw. Julius Mtatiro, alisema hilo ni pigo kubwa kwa CUF na UKAWA hasa kipindi hiki cha kutafuta ushindi katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, mwaka huu.
 
Kwa mujibu wa ujumbe wake alioutuma kwenye akaunti yake ya Facebook, Bw. Mtatiro alisema uamuzi huo ni mgumu kwani hajawahi kuusikia tangu awe mwanachama wa CUF miaka nane iliyopita.
 
Alisema kidemokrasia lazima kukubali matokeo na uamuzi binafsi wa mtu yeyote kwani mwisho wa siku, mtu hufanya uamuzi wake na tunalazimika kuyaheshimu ili maisha yaendelee.
 
 Aliongeza kuwa, si vizuri kumshutumu Prof. Lipumba kwenye mitandao na kwingineko bali akumbukwe kwa mchango wake mkubwa kisiasa ambapo jemedari anapoanguka vitani bunduki yake huchukuliwa na vita kuendelea. 

ACT-Wazalendo Yachomoza Katika Majimbo 203


CHAMA cha ACT – Wazalendo kimesema hadi sasa wamejitokeza wagombea katika majimbo 203 ya uchaguzi nchini huku kura za maoni za kupata wagombea katika majimbo mbalimbali zikiendelea.

Madiwani 18 wa CCM Wahamia CHADEMA


Madiwani 18 wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wametangaza kuhama chama hicho jana jijini Arusha.
 

Madiwani hao waliotangaza kuihama CCM walikuwa katika ofisi za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wilayani Arumeru.

Huku aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Elias Ngorisa aliyefuatana na Diwani wa Kata ya Engusero Sambu, Kagil Mashati Ngukwo, ambaye pia alikuwa Katibu wa Fedha na Uchumi wa CCM Wilaya ya Ngorongoro naye pia amejiunga na Chadema.

Walikuwepo wazee wa mila wa Kabila la Wamasai (malaigwanani) Laurence Ngorisa na Lekakui Oleiti, wote kutoka Engusero Sambu. Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari, ndiye aliyewapokea makada hao na kuwapatia kadi za Chadema.

Akizungumza baada ya kupokea kadi, Elias Ngorisa, alisema wapo madiwani 18 kati ya 28 ambao tayari wamechukua kadi za Chadema na kuondoka CCM na watatetea nafasi zao kupitia Chadema katika uchaguzi wa Oktoba mwaka huu.

Alisema yapo mabadiliko makubwa na Watanzania hawana budi kuyakubali na ameshawishika kubadilisha mwelekeo toka CCM kwenda Chadema.
 

Kwa upande wake, Diwani Ngukwo, alisema, amekihama chama hicho kwa sababu anahitaji mabadiliko na anaamini wengi watawafuata ili waweze kuondokana na manyanyaso mengi ya Loliondo wanayopata.

Wednesday, August 5, 2015

Madereva watangaza mgomo mwingine nchi nzima


Mgomo mwingine wa madereva nchini Tanzania unanukia  kufuatia Chama cha wafanyakazi madereva Tanzania-TADWU pamoja na wizara ya kazi kushindwa kutekeleza makubaliano yayolifikiwa na tume iliyoundwa na waziri mkuu kutatua mgogoro huo.
 
Kwa mujibu wa naibu katibu mkuu wa TADWU, Bwana Rashidi Salehe amesema kwamba kutokana na Wizara kushindwa kutekeleza makubaliano hayo wanatarajia kugoma tena  kuanzia Agosti tisa mwaka  huu.
 
Amesema  kuwa madereva watagoma tena kufuatia wizara ya  kazi pamoja na Sumatra kuendelea kutumia mikataba ya zamani katika kutoa leseni wakati makubaliano ya tume iliyoundwa na waziri mkuu yalitaka mikataba mipya ianze kutumika kuanzia julai mosi mwaka huu.
 
Katika makubaliano  yao mapya, madereva wa malori yanayotoka nje ya nchi walikuwa wanatakiwa kulipwa mishahara ya shilingi milioni moja, huku madereva wa daladala shilingi laki tano pamoja na posho.

Magufuli Alitikisa Jiji la Dar es Salaam Wakati Akichukua Fomu ya Kugombea Urais


Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Cham cha Mapinduzi (CCM),Dkt  John Pombe Magufuli na Mgombea Mwenza Ndugu Samia Suluhu Hassan wakionesha fomu zao za kuomba kugombea urais mara baada ya kuchukua kwenye ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi jijini Dar es salaam leo, ambapo walisindikizwa na viongozi mbalimbali pamoja na wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla wakiwa wamepanda kwenye gari maalum.