Thursday, September 17, 2015


Staa wa filamu Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ ameendelea kushusha maneno kwa chama kinachounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) baada ya kufunguka hadharani kuwa hawakuwa na sera ambazo zingemfanya aendelee kubaki.


Staa huyo ambaye kwa sasa amerudi Chama Cha Mapinduzi (CCM) amesema kurudi kwake CCM hakumaanishi kama amehongwa kama watu wanavyoendelea kusambaza habari hizo bali amekwenda kutokana na kuvutiwa na sera.

LOWASSA: Asanteni Chato Kwa Mahaba Matamu.....Mnanifanya Nideke


Mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, anayeungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Watanzania (Ukawa), ameipenya ngome ya mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, wilayani kwake Chato na kupata mapokezi makubwa.


Mkutano wa jana ulikuwa wa kwanza kufanyika mjini hapo akiwa ametokea Morogoro, mkutano mwingine aliufanya mjini Geita.

Wednesday, September 16, 2015

Mitambo ya Kuzalisha Umeme wa gesi Yawashwa.....Tatizo la Umeme Kukatika Kuisha LEO.


Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limesema kazi ya kuunganisha mabomba ya gesi kutoka Kinyelezi I kwenda katika mitambo ya Ubungo I na II, jijini Dar es Salaam imekamilika.

Aidha, kazi ya kuwasha mashine 10 za mtambo wa Ubungo I imekamilika na  inategemewa tatizo la kukatika umeme litafikia tamati kuanzia leo.